Psalms 64:2-5

2 aUnifiche kutokana na shauri la siri la waovu,
kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.

3 bWananoa ndimi zao kama panga
na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 cHurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia,
humrushia ghafula bila woga.

5 dKila mmoja humtia moyo mwenzake
katika mipango mibaya;
huzungumza juu ya kuficha mitego yao,
nao husema, “Ni nani ataiona?”
Copyright information for SwhNEN